Tarehe 19 mwezi Novemba, ni siku itakayokumbukwa siku zote na Kampuni ya ABC Bicycle pamoja na wateja wake.

Baada ya siku 5 za kazi kufungwa kwaajili ya maandalizi ya tukio hilo kubwa, Jumamosi ya tarehe 19 Novemba inaingia kwenye historia ya siku kubwa kwa mwaka 2022.

Mafundi waliwekeze muda mwingi kuandaa Baiskeli nyingi kwaajili ya mauzo hayo makubwa, na hivyo huduma kama urekebishaji wa Baiskeli za mteja mmoja mmoja kusimama.

Jumla ya Baiskeli 400 zilifungwa ndani ya siku 5, ambapo ni wastani wa Baiskeli 80 kwa siku.

Tunapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru wateja wetu wote waliofika kwaajili ya Mauzo hayo makubwa. Vilevile tunawakumbusha wale wote ambao hawakuweza kufika, kuendelea kufika katika Ofisi yetu ya Moshi na Arusha kwani Baiskeli bado zipo na ni nzuri sana.

Tembelea ukurasa wetu wa Facebook na Instagram @abcbicyclecompanyltd au wasiliana nasi kwa simu 0764056791(Arusha) na 0757559141(Moshi)

 

Previous Post
Newer Post

Leave A Comment

No products in the cart.

X